Nov 26, 2012

R.I.P Sharo-Milionea




Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Constatine Masawe amekiri kutokea kwa msiba wa Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’, baada ya kupata ajali katika kijiji cha Lusanga, Muheza akiwa katika gari lenye namba za usajili T478 BVR Toyota Harrier, majira ya saa mbili usiku, ambapo pia ndio nyumbani kwao.

Sasa naweza kusema R.I.P Sharomilonea. Maiti ya Sharo Milionea imehifadhiwa hospitali ya Teule Muheza.

Kuhusu Habari ya Mazishi tutataarifiana tupatapo updates kutoka kwa Ndugu wa karibu

PERUZZI NA MIMI IPO PAMOJA NA NYI MLIOGUSWA NA MATATIZO HAYA, NA KUMUOMBEA KWA MUNGU AMPOKEE.. BWANA ALITOA NA BWANA ALITWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE SASA NA HATA MILELE AMEN.


Peruzzi na Mimi.

No comments: