Dec 29, 2011

CloudsTV wanauharibu wimbo wa Taifa la Tanzania


Kuna wimbo ambao Television ya Clouts imekuwa ikiuweka kila mara, huku
selikali ukiusikiliza bila kuchukua hatua yeyote ile, ni mchafu na
haufuati taratibu za wimbo wa Taifa unaoheshimika na kila mtu hapa
Tanzania.

Kwanza haukuimbwa kama ulivyo wimbo ule tunaouheshimu sisi Watanzania,, hii sasa nini tunafanya

naomba tuwe serious katika mambo ya msingi wimbo wa Taifa si wa
kuuchezea...

Career Leo





Silvanus

New Career



Winrock 
International
Putting ideas to work

location: tabora, tanzania

position title: monitoring & evaluation (m&e) officer for promoting sustainable practices to eradicate child labor in tobacco (prosper) project

position summary: the monitoring and evaluation (m&e) officer is a key personnel position for the promoting sustainable practces to eradicate child labor in tobacco (prosper) project to combat exploitive child labor in tanzania. the m&e officer will oversee the implementation of the project's monitoring and evaluation strategies and requirements. the m&e officer will be responsible for developing and maintaining and training teams in the child labor monitoring system (clms) and the project data base and for reporting on indicators and beneficiaries for the quarterly progress reports. .

specific responsibilities include but are not limited to:
         it design and implement a comprehensive monitoring and evaluation system including child labour monitoring and tracking.
         maintain and report all children withdrawn and prevented from child labor for direct beneficiaries.
         design and train staff and project team in community based monitoring and data collection.
         design data collection instruments, schedules, analysis methods and applied technologies and
         utilize existing tools to be provided by the project as appropriate.
         developing and managing project database for data collected from communities, including the

project database and/or the clms.
         establish and train community activists, community monitoring committees and government officials
         as data collectors.
         liaise with external monitoring and evaluation teams for mid-term and final evaluations.
         assist the project director in the country child labor monitoring system (clms) to harmonize the
         prosper data base with the clms and possible international labor organization and ministry of education data bases
         develop, conduct and/or supervise pre-and post-awareness raising assessments and periodic community surveys as relevant
         other related m&e tasks as appropriate

qualifications:
         at least three years progressively responsible experience in the monitoring and evaluation of
·         international development projects in child labor, education and training or a related field. related experience can include strategic planning and performance measurement, indicator selection, quantitative and qualitative data collection and analysis methodologies, database management, and knowledge of reporting on child labor incidences.

         experience training and building the monitoring and evaluation capacity of team members, partners, government stakeholders, school officials and community monitoring committees highly desired.
         masters degree or equivalent in social sciences or specialized training/certification in monitoring and evaluation preferred.
·         fluency in english and one other local language required.
         willingness and ability to commit to starting the position within 30 days of the offer in or around february 2012.

application:
i applicants should send11it il'teir resume and cover letter to rocio cordova at rcordova@winrock.org, by january 10, 2012 

Silvanus

PERUZI NA MIMI: Vacancies

PERUZI NA MIMI: Vacancies

Silvanus

Vacancies


Amana Bank Tanzania Vacancies

AMANA BANK TANZANIA JOBS

SEND YOUR CVS TO

Amana Bank Limited,
Garden/Ohio Street PPF Tower 3rd floor,
P.O. Box 9771,
T: +255 22 2129007/8
E: info@amanabank.co.tz
Dar es Salaam, Tanzania

Dec 27, 2011

He Kills his childrens because of their dispute with his wife

One citizen in Ivory Coast, who is living in England (Jean Francis Say) recently made ​​genocide for pressing collar throats his two children until death. 
The incident occurred south Southwark east of London, is said occurred after a dispute between two of him and his wife,
His wife who had left home their  Children after the dispute, she come back after a few days later when they met again
He take his children and he did the same inhuman and then call his wife to come and take the dead bodies of his sons the male Rolls 10-year-old Regina girl eight years old.

Silvanus

20 GOLDEN RULES FOR 2012.


There is one key factor that can either damage your relationships or deepen them. That factor is your attitude. If you’re hoping to grow and maintain positive relationships in your life

1. Stop holding grudges. – Grudges are a waste of perfect happiness.

2. Stop complaining. – Instead, use your time and energy to do something about it.

3. Stop meaning what you don’t say. – People can’t read minds. Communicate regularly and effectively.

4. Stop making it all about you. – The world revolves around the sun, not you. Take a moment to acknowledge this truth on a regular basis.

5. Stop lying. – In the long-run the truth always reveals itself. Either you own up to your actions or your actions will ultimately own you.

6. Stop blaming. – Blaming others accomplishes nothing. Either you own your problems, or they will own you. Your choice. When you blame others for what you’re going through, you deny responsibility – you give-up your power over that part of your life, and you annoy everyone around you in the process.

7. Stop doubting. – If you think that you can’t achieve something, I have some news for you, you’re probably right. But don’t let your self-doubt interfere with other people’s dreams. Remember, the one who says it can’t be done should never interrupt the one doing it. (Read Unstoppable.)

8. Stop interrupting. – Correcting someone when they’re blatantly wrong is one thing, but always interjecting your opinions out of turn gets old fast.

9. Stop being selfish. – You get what you put into a relationship. Nothing less, nothing more.

10. Stop judging. – Everyone is fighting their own unique war. You have no clue what they are going through, just like they have no clue what you’re going through.

11. Stop gossiping. – Gossiping about others is a lose/lose situation. It hurts them, and then it hurts your reputation.

12. Stop making promises you can’t keep. – Don’t over-promise. Over-deliver on everything you do.

13. Stop being defensive. – Just because someone sees something differently than you doesn’t mean either one of you is wrong. Keep an open mind. Open minds discover great things.

14. Stop comparing people to others. – No two people are alike. Everyone has their own strengths. We are only competing against our own selves.

15. Stop expecting people to be perfect. – ‘Perfect’ is the enemy of ‘good.’ And genuine ‘goodness’ is hard to find in this world. Don’t overlook it.

16. Stop trying to be everything to everyone. – It’s impossible. But making one person smile can change the world. Maybe not the whole world, but their world. So narrow your focus.

17. Stop screwing people over just because you can get away with it. – Just because you can get away with something doesn’t mean you should do it. Think bigger. Do what you know in your heart is right. (Read Life’s Greatest Lessons.)

18. Stop making mountains out of molehills. – People make mistakes. Crap happens. There’s no reason to stress out yourself and everyone around you because of it. One way to check if something is worth mulling over is to ask yourself this question: “Will this matter in one year’s time?” If not, then it’s not worth worrying about.

19. Stop being dramatic. – Stay out of other people’s drama and don’t needlessly create your own.

20. Stop giving out advice, and just listen. – Less advice is often the best advice. People don’t need lots of advice, they need a listening ear and some positive reinforcement. What they want to know is already somewhere inside of them. They just need time to think, be and breathe, and continue to explore the undirected journeys that will eventually help them find their direction.

*** And remember, your relationship with yourself is the closest and most important relationship you will ever have. So pay attention to it, develop it, nurture it, and never, ever stop.

Silvanus

Dec 26, 2011

TAARIFA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA, MVUA KUENDELEA

KUTOKA MAMLAKA YA HALI YA HEWA

Kutokana na ongezeko la mvua zinazoendelea katika maeneo mengi nchini Mamlaka ya Hali ya Hewa inatoa taarifa ya mwelekeo wa mvua hizo katika kipindi cha siku kumi zijazo kuelekea mwaka mpya 2012.

Mifumo ya hali ya hewa inaonyesha kuimarika kwa hali ya joto la Bahari ya Hindi, sambamba na kuongezeka kwa msukumo wa hewa yenye unyevunyevu kutoka misitu ya Kongo na kusababisha makutano ya upepo katika eneo la mashariki na kusini magharibi mwa nchi.

Hali hii inatarajiwa kuendelea kusababisha vipindi vya mvua kubwa katika maeneo ya Mikoa ya Pwani ya kasikazini (Morogoro, Pwani, Dar es Salaam, Tanga na kisiwa cha Unguja) hadi tarehe 22 Disemba 2011. Mvua hizo zinatarajiwa kurejea katika hali ya kawaida kuanzia tarehe 23 Disemba katika maeneo hayo.

Aidha maeneo ya mikoa ya nyanda za juu kusini magharibi( Mikoa ya Mbeya, Iringa na Sumbawanga), kanda ya kati (Mikoa ya Dodoma na Singida) na magharibi mwa nchi (Mikoa ya Kigoma na Tabora) yanatarajiwa kuendelea kuwa na mvua katika kiwango cha juu ya wastani pamoja na vipindi vya mvua kubwa. Hali hii inakwenda sambamba na utabiri wa mvua za Vuli na za Msimu ambapo maeneo mengi ya nchi yalitarajiwa kuwa na mvua juu ya wastani na vipindi vya mvua kubwa.

Kulingana na viwango vya mvua zilizonyesha katika kipindi kifupi ongezeko kidogo la mvua katika maeneo hayo linatarajiwa kuendelea kusababisha mafuriko na uharibifu wa miundombinu. Mamlaka inashauri tahadhari stahiki ziendelee kuzingatiwa.

Maeno mengine ya nchi yanatarajiwa kupata mvua za kawaida katika kipindi hicho. Aidha mwelekeo wa mvua katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari 2012 utatolewa mwishoni mwa mwezi huu.

Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia mwenendo wa mifumo ya Hali ya hewa na athari zake na itaendelea kutoa taarifa na tahadhari kila inapobidi.

Dk. Agnes L. Kijazi
MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA HALI YA HEWA
TANZANIA

Dec 20, 2011

Flood in Dar es salaam


Huyu mbunge ni mfano wa kuigwa.. Jiji la Dar es Salaam lina wabunge wasiopungua watano.. Lakini hakuna hata mmoja aliyekunbuka kusaidia kazi uokoaji katika maafa ya Mafuriko, ila Mbunge huyu wa Mafia Mh. Abdulkarim Shah, aliye jitolea Boti na yeye mwenyewe kuthubutu kuingia kazini kama munavyo muona kwenye picha... Wabunge wetu acheni usharobaro.




JIJI la Dar es Salaam na vitongaji vyake, limekumbwa na maafa ya vifo vya watu watano akiwamo mmoja aliyepigwa na radi, uharibifu wa miundombinu huku mamia ya watu wakikosa makazi, kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia jana.Mvua hizo zilisababisha tatizo kubwa la usafiri kutokana na barabara kujaa maji, kuezua nyumba na kuua watu watano na kuacha maelfu ya wakazi wa jiji hilo bila makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa mapaa.

Mvua hiyo ilianza kunyesha mnamo saa 9:00 alfajiri ikiambatana na radi na ngurumo nzito na kusababisha kukatika mara kwa mara kwa umeme katika baadhi ya maeneo ya jiji hilo ambalo ni kitovu kikuu cha biashara na uchumi kwa nchi.

Waandishi wa gazeti hili waliotawanyika sehemu mbalimbali za jiji hilo, walishuhudia maiti za watu wawili waliozolewa na maji maeneo ya Sinza na Msewe.

Wakati maiti moja ikitambuliwa kwa jina la Ibrahimu Lusama (60), maiti nyingine ambayo ilipatikana katika Bonde la Mto Ng'ombe bado haijatambuliwa.

Hata hivyo, moja ya maiti hao alisemekana anatoka eneo la Msewe na aliokotwa eneo la Sinza Iteba, takriban umbali wa kilometa tano. Madaraja ya Msewe na Sinza Iteba yalivunjika na kusababisha usumbufu mkubwa kwa abiria wanaotumia madaraja hayo.

Madaraja mengine yaliyovunjika ni pamoja na daraja la Msewe na la mto wa Ng’ombe, huku magari yaliyokuwa yakienda Mwananyamala, Mikocheni yakitokea Ubungo yakilazimika kusitisha safari zake baada ya kujaa maji.

Baadhi ya maeneo ya jiji hasa Kigogo, Tandale, Mabibo na Tabata yalikumbwa na kadhia ya maji kujaa kwenye makazi yao na kusababisha usumbufu ambao ulionekana kutishia usalama wa mali na maisha.

Wazee walikuwa wakihangaika huku na kule kutafuta sehemu za kujisitiri, lakini vijana na watoto walionekana wakicheza kwenye mvua bila kujali mustakabali wao.



Wafanyabiashara wa vyakula vya jumla na rejareja katika baadhi ya maeneo waliamka na kukuta sehemu kubwa ya bidhaa zao zimeharibika huku meza na vyombo vya mama lishe, vikionekana kuelea barabarani baada ya kusombwa na maji.

Sinza
Mawasiliano ya Sinza na Tandale yalikatika baada ya daraja kusombwa na maji huku maiti ya mtu aliyeonekana kuwa mzee wa makamo ukikutwa umekwama kwenye kingo za daraja, kabla ya kuokolewa na wasamaria wema.

Mmoja wa wamiliki wa zahanati moja iliyoko Kigogo Darajani ambaye jina lake halikufahamika mara moja, alisema amepata hasara baada ya maji kuingia ndani na kuharibu vifaa mbalimbali vya hospitali zikiwamo dawa.

"Angalia, nimepata hasara sana. Mpaka sasa wasaidizi wangu wanafanya kazi ya kuzoa maji na kusafisha vitanda na baadhi ya vifaa, vingine havifai," alisema mmiliki huyo ambaye hakuwa tayari kutaja jina.

Katibu wa CCM tawi la Kigogo Wakereketwa, Charles Gumbo alisema kulikuwa na taarifa za watoto ambao hakuwataja idadi kufariki, baada ya mama yao kuwapandisha juu ya kabati kwa lengo la kuwaokoa.

Hata hivyo, kabati hilo na nyumba walimokuwa ikiishi familia hiyo vilisombwa na maji huku mama wa watoto hao akikimbia kutafuta jia ya kujiokoa.

"Hapa tunachambua mboga kutayarisha chakula cha mchana, lakini hatujui usiku itakuwaje...mvua zenyewe ndiyo kama hizi," alisema Joyce Meshack huku akionyesha kukata tamaa.

Msimbazi na hosipitalini
Mwananchi pia ilishuhudia watu kadhaa wakiwa wanaopolewa katika daraja la Mto Msimbazi, baada ya kuzolewa na maji na kukimbilia kwenye miti ya mpapai. Kazi hiyo ilifanywa na Kikosi cha Uokoji cha Polisi.

Helkopta za Polisi na Jeshi la Wananchi (JWTZ) zilionekana angani zikiwa zinafanya doria katika maeneo yalioyodhurika kutokana na mafuriko hayo.

Katika Hospitali ya Manispaa ya Ilala (Amana), watu kumi walifikishwa kwa ajili ya matibabu baada ya kuopolewa kwenye maji maeneo mbalimbali ya manispaa hiyo.

Mganga anayeshughulikia maafa katika hospitali hiyo, Christopher Mzava alisema majeruhi hao waliofikishwa hospitalini hapo kwa nyakati tofauti kuanzia saa 12:00 asubuhi jana.

Katika Hospitali ya Temeke mtu aitwae Gate Mseti ameokotwa baada ya kupigwa na radi huku akiwa na mtoto Thobias Rashid (6) ambaye amejeruhiwa.

Muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo, Senzota Khalifa alisema wamepokea watu wawili mmoja akiwa amekufa huku mtoto aliyekuwa amejeruhiwa akiruhusiwa na kuongeza kwamba, maiti hiyo ilipelekwa hospitalini hapo na wasamaria wema wakiongozwa na polisi aliyejulikana kwa jina la James. 

Katika Hospitali ya Mwananyamala, kulipelekwa maiti watatu na majeruhi wawili na mmoja kati yao alipelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.

Katibu wa Afya wa Hospitali hiyo, Edwin Disakara aliwataja marehemu hao kuwa ni Ibrahim Lusama wa Ubungo Maji (60), Vivian Maximilan wa Mburahati (13) na mtoto mmoja mwenye umri wa miezi kadhaa aliyeokotwa kwenye tope.

Alisema majeruhi ni Hawa Yusuf mkazi wa Tandale na Tatu Juma ambaye baadaye alipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Polisi na Serikali ya mkoa
Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Suleiman Kova alithibitisha vifo vya watu watatu akieleza kuwa vyote vimetokana na mvua hizo.
Alitaja waliofariki kuwa ni mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Jackline (33), ambaye ni Mkazi wa Kitunda. Alisema mwanamke huyo alikufa baada ya kupigwa na radi akiwa amempakata mwanaye, lakini mtoto alipona.
Kwa mujibu wa Kova, wengine waliofariki dunia ni Maganga Said (8) Mwanafunzi na Mkazi wa Kiwalani ambaye alikanyaga waya wa umeme uliokuwa umeanguka chini na Ibrahimu Lusama (60) aliyefariki baada ya kuzolewa na maji katika daraja la Msewe.
Kova aliwataka wakazi wanaoishi mabondeni kuondoka mara moja kupisha mvua hizo ambazo Mamlaka za Hali ya Hewa imesema zitaendelea kunyesha mfululizo kwa siku kadhaa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick alithibitisha vifo hivyo na kueleza kuwa maiti ya mtu aliyetambuliwa kwa jina la Lusama, alizolewa na maji kutoka daraja la Msewe mpaka Mto wa Ng’ombe.

"Hali ni mbaya sana kwa jiji la Dar es salaam, kwani watu wamepoteza maisha na makazi yao pamoja na mali," alisema Sadick na kuongeza:

“Tulishatangaza watu wahame mabondeni jamani, lakini bado wanaendelea kukaa tu huko na haya ndio matatizo yenyewe,”alisema

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana, ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya za Ilala na Temeke, alisema katika wilaya zote tatu, wilaya ambayo imeathirika zaidi ni Kinondoni ambako kumetokea maafa.

“Kinondoni ndiko hasa kulikotokea maafa makubwa, wilaya nyingine ni salama,”alisema Rugimbana.



Utabiri wa TMA
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mvua hizo zitaendelea kunyesha mfululizo kwa siku mbili zaidi.



Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Agness Kijazi alisema jana kuwa, mvua hizo zimesababishwa na upepo kutoka nchi za Kongo na Msumbiji unaopeleka joto katika Bahari ya Hindi.



Alisema mvua hizo zitaendelea kunyesha kutokana na wingu zito lililotanda katika maeneo ya Pwani ya Kaskazini ya mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro,Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba. 
Maeneo mengine ni mikoa ya Singida, Dodoma, Mbeya na Iringa.
"Wingu hilo limesababisha mvua kubwa ambayo inaendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo hayo kwa hali hiyo inatarajiwa kuendelea kwa muda wa siku mbli zijazo"alisema Kijazi.





Rescuers wade in the floodwater to save a person who had sought refuge on a tree at the Kigogo valley in Dar es Salaam yesterday morning.  

Flood result

People suffered alot