Jan 4, 2012

Child is taking care for his Mothers Child for His Mothers Sick at Muhimnili Hospital


No one regrets the birth, many have been pleased with
expecting a good life, but the child Mustapha Ali (12) (pictured) has
been different.

The child, who is a resident of Mtoni Mtongani Temeke District, in
Dar es Salaam, who studied standard six is the first baby born in
their families and is now faced with the burden of having nurse a sick person and taking care of the twins, and Ramadan Swaumu aged eight months.

These children have been admitted at Muhimbili National Hospital and child
Mustapha has promised to take care of his mother until she recover.

Mustapha, has left the role  of nurse his mother who is sick after their father He died.


"Father had been engaged in the work of laborers and mother of his work is
street selling vegetables. They enable us to make ends meet, for each
day and pay the rent.





Hakuna mtu anayejutia kuzaliwa, wengi wamekuwa wakifurahia huku wakitegemea maisha mazuri lakini kwa mtoto Mustapha Ali (12) (pichani) imekuwa ni tofauti.

Mtoto huyo ambaye ni mkazi wa Mtoni Mtongani Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam anayesoma darasa la sita ni wa kwanza kuzaliwa katika familia yao na kwa sasa anakabiliwa na mzigo wa kuwauguza wadogo zake mapacha, Swaumu na Ramadhani wenye umri wa miezi nane.

Watoto hao wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na mtoto Mustapha ameahidi kuwa atawauguza wadogo zake hadi wapone.

Mustapha, amebaki na jukumu hilo baada ya mama yao aliyekuwa akiwauguza wadogo zake kuugua na kwa sasa yupo mahututi, wakati baba yao alishafariki dunia.

Mtoto huyo anayewauguza wadogo zake katika wadi ya watoto, Makuti B, wiki iliyopita alizungumza na mwandishi wetu na alikuwa na haya ya kusema:

“Maisha yamebadilika ghafla na kuwa mabaya hasa baada ya baba kufariki dunia nikiwa na miaka minne.

“Baba alikuwa akijishughulisha na kazi za vibarua na mama kazi yake ni kuuza mboga mitaani. Kazi hizo zilituwezesha kupata mahitaji ya kila siku na kulipa kodi ya nyumba.

“Mwaka 2007 baba alifariki dunia tukabaki na mama ambaye aliendelea na shughuli na biashara yake. Alikuwa akifanya kazi hiyo bila kupumzika, mzigo wa maisha ulimlemea, nikakatisha kwenda shule nikawa nabaki nyumbani kumsaidia.

“Kufuatia kifo cha baba, muda mwingi mama alionekana mnyonge na aliyejaa mawazo mengi kutokana na kazi ngumu, wakati mwingine alikuwa akitokwa machozi.

“Mwaka juzi mama alipigiwa simu na kuambiwa kuwa bibi anaumwa huko Kigoma na hana mtu wa kumuuguza, ilimbidi aende hata hivyo, hakupona alifia mikononi mwake na baada ya mazishi alirejea Dar na kukuta kodi ya nyumba imeisha.

“Licha ya kusumbuliwa na maradhi, aliendelea na biashara yake kwani hakukuwa na mtu wa kumtegemea, alikuwa akiniambia bila kwenda kwenye shughuli hizo, tungekufa na njaa.

“Mama alianza kuchanganyikiwa kimawazo pale Swaumu na Ramadhan walipoanza kuumwa, alikuwa haendi kuuza mboga. “Maisha yalikuwa ni magumu, tulikuwa tukisaidiwa chakula na wasamaria wema wakati mwingne tulishindia uji.

“Hali za kiafya za wadogo zangu hawa (akiwaonyesha kwa mwandishi), zilianza kuwa mbaya na mama akawa hana fedha za kuwapeleka hospitali.

“Novemba 11, mwaka jana aliamua kuwaleta hapa Muhimbili akiwa hana fedha.
“Alimweleza daktari matatizo yaliyokuwa yakitukabili kiafya na kiuchumi ndipo wadogo zangu walipokolewa na kuanzishiwa matibabu.

“Wadogo zangu walilazwa hapa mimi nilirudi nyumbani na majirani wakawa wanapika huko kwao na kunipa mimi nikawa namletea mama hapa hospitali.

“Niliendelea na zoezi hilo kila siku, nikashindwa kwenda shule lakini niliamini kuwa ipo siku wadogo zangu wangepona nami ningeendelea na masomo.

“Hali ya mama ilizidi kuwa mbaya kuliko hata wadogo zangu akawa anapatiwa, afya yake ilizidi kudhoofu daktari akashauri apewe dawa za kutumia akiwa nyumbani, akarudi nyumbani.

“Hakukuwa na ndugu wa kubaki na wadogo zangu hospitalini, hivyo nikaamua niwauguze, nimekuwa nikilala nao kitanda kimoja.

“Kinachonihuzunisha ni kwamba, sielewi mama anaendeleaje na jambo lingine linaloniumiza kichwa ni
kwamba kodi ya nyumba imekwisha mwezi uliopita, sijui tutapata wapi fedha katika hali hii!.

“Mama hana nguvu tena ya kujishughulisha, hatuna ndugu wa kumwangalia ningekuwa na uwezo ningempeleka kwetu Kigoma.

“Nina mawazo mengi kwani hata kama akipatikana mtu wa kubaki na wadogo zangu hapa hospitalini nitaendaje shule? Sina viatu, nguo na madaftari nitaishi wapi na nitakula nini?

“Hata wadogo zangu hawana nguo na mahitaji mengine muhimu.Tunaomba mtu yeyote mwenye huruma atusaidie kutulipia kodi ya nyumba, chakula na nguo ili tuweze kujinusuru na hali ngumu inayotukabili,” alisema mtoto Mustapha huku akitokwa machozi.
Mtu yeyote aliyeguswa na kilio cha mtoto huyo amtembelee Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kama una uwezo, itapendeza ukimsaidia, kwani anahitaji msaada wa hali na mali.

No comments: