Jan 13, 2012

RIP Mzee Kipara

Mara kadhaa Mzee Kipara alilalamika kusumbuliwa na miguu ambayo ilikuwa ikivimba ambapo kwa mujibu wa daktari wa Ijumaa, kilichomuua ni high blood pressure inayosababisha moyo kupanuka na kushindwa kufanya kazi, kitaalamu huitwa Congestive Cardiac Failure (CCF).
Hali hiyo husababisha moyo kushindwa kusukuma maji kutoka chini kwenda juu, hivyo miguu kuvimba na ugonjwa huo kitaalamu huitwa Oedema.

‘BURIANI Mzee Kipara!’ Ndiyo maneno yanayoweza kumtoka binadamu yeyote aliyeshuhudia maisha ya mateso ya mzee huyo kabla ya kukutwa na mauti, aya zifuatazo zinaweza kukutoa machozi.
Fundi Said maarufu kwa jina la Mzee Kipara, alikuwa msanii mkongwe katika tasnia ya uigizaji Bongo, aliyetumia sehemu kubwa ya maisha yake katika sanaa ambaye juzi (Jumatano), Januari 11, mwaka huu, saa 2:00 asubuhi, Mungu alimchukua baada ya maumivu ya muda mrefu.
Mzee Kipara aliyeanza kusikika kwenye maigizo ya Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD, sasa TBC Taifa), alifariki dunia katika nyumba aliyokuwa amepangishiwa na Kundi la Sanaa la Kaole iliyopo Kigogo Mbuyuni, Dar es Salaam.

No comments: