May 17, 2019

SILVANUS MUMBA: PANGA MALENGO YAKO KWA KUTUMIA SMART OBJECTIVES



Silvanus mumba Vijana wengi na wafanya biashara wengi, wale wa Biashara ndogondogo na zile biashara kubwa, hawapendi kupanga malengo yao, na ndio maana biashara zao zinakuwa sio za uhakika. utaenda mwaka huu utamkuta akiuza samaki, mwakani anauza karanga, kwasababu hawana mipango na hawajui jins ya kuifanya iwe mipango endelevu.

Peruzzi na Mimi.

Apr 12, 2019

SILVANUS MUMBA: USIPOKUWA MUAMINIFU HUWEZI KUPATA WASHIRIKA KIBIASHARA


Silvanus Mumba ni Professional Human Resources Manager with since 2009 working as Administrator (KOICA) Program Coordinator (KOICA) HR Officer (Vipajilink) HR Manager (CRSG) HR Manager (Sunshine Mining) and HR Consultant (Hadithi Zetu Limited)

Silvanus Mumba is a Gospel artist and Motivational speaker too, doing his Motiations jobs through Video Podcasts on his YouTube channel, Here is his one of the Motivation Videos.
 Peruzzi na Mimi

Jan 1, 2019

TAGOANE LOAN Fund yazinduliwa na Mh. Juliana Shoza


Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza  akitoa wito kwa wasanii wote nchini kujiunga na Mfuko wa Mkopo wa TAGOANE (TAGOANE LOAN FUND) unaoratibiwa na Taasisi ya Tanzania Gospel Artists Network (TAGOANE) leo Jijini Arusha, alipokuwa akizindua mfuko huo ambapo amesisitiza kuwa  wasanii wa makundi yote wanaweza  kujiunga wakikidhi masharti ya kujiunga.


Naibu  Waziri  Mhe.Juliana Shonza ametoa wito kwa  wasanii kujitokeza na kujiunga na Mfuko wa Mkopo wa TAGOANE LOAN FUND, leo Jijini Arusha  alipokuwa akizindua Mfuko Mkopo wa TAGOANE  LOAN  FUND katika Tamasha la Tukuza Festival  lililoandaliwa na Tanzania Gospel Artists Network (TAGOANE).

Walio vaa scafu za Scout Tanzania ni Kushoto kwa Mh. Juliana Shoza ni Mwanasheria wa TAGOANE Dr. Laltaika, anayefuata Dr. Godwin Maimu Raisi wa Tagoane na Kulia kwae ni Ndugu Silvanus Mumba KAtibu Mkuu Mwenza.

 “Tumekuwa tukishuhudia wasanii wengi wenye majina makubwa wakikosa fedha hata za matibabu  hili limekuwa ni suala lisilo pendeza hivyo ni vyema wasanii mkajiunga katika mfuko huu ambao utawasadia kupata mikopo yenye riba nafau na bima ya afya kupitia hili mnaweza kujikwamua kiuchumi  na kujifunza kuwekeza kwa maisha ya baadae ,“alisema Mhe.Shonza.

Kwa Upande wa Rais wa TAGOANE  Dkt.Godfrey Maimu alifafanua kwamba mfuko huo haubagui msanii kwani  msanii yeyote anayetaka kujiunga anaruhusiwa  kwani lengo la mfuko huo ni kuimarisha umoja wa wasanii na kuhakikisha maisha ya msanii yanaenda kubadilika badala ya msanii kuonekana ni mtu tegemezi  na wakuomba kusaidiwa hata kwenda studio kurekodi.

“TAGOANE tumekuwa tukifanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kusaka vipaji vya uimbaji kwa watoto yatima ambapo lengo ni kuwasadia katika kukuza vipaji vyao lakini  pia na kuwasimamia masuala ya shule katika kuhakikisha  wanapata mahitaji yote muhimu ya shule,”alisema Dkt.Maimu.
Kwa upande wa Katibu Mwenza wa TAGOANE Bw.Silvanus Mumba alieleza kuwa Tamasha hilo kwa mwaka huu limemeendesha Semina ya siku mbili kwa wasanii kuhusu masuala ya Sheria,Sanaa na Ubunifu lengo likiwa ni kumjenga msanii kuendesha shughui zake kwa weledi.


Halikadhalika nae Mmoja wa watoto yatima kutoka Wilaya ya Siha ambaye ni yatima mwenye kipaji cha kuimba nyimbo za injili Witness Justine aliushukuru uongozi wa TAGOANE kwa kumuahidi kumpeleka studio kurekodi nyimbo zake pamoja na kuzitangaza nyimbo hizo pia aliwashukuru kwa kuibua Kipaji chake

Peruzzi na Mimi.

Sep 2, 2018

NITASUBIRI - SILVANUS MUMBA



Muimbaji wa nyimbo za injili anasema "Niliuimba wimbo huu nikiwa na stress nyingi sana, lakini kupitia huu wimbo nimeweza kupata maono makubwa sana ya kuwahudumia watu."

Endelea kumfuatilia kupitia Youtube channel yake kwa Mafundisho mbali mbali anayoyaweka na nyimbo zake


Peruzzi na Mimi.

NURU - SILVANUS MUMBA (Official video)

Peruzzi na Mimi.

Dec 28, 2017

MTUMISHI WA MUNGU SILVANUS MUMBA AACHIA NURU

Muimbajiwa Nyimbo za Injili Tanzania ametoa Albam yake ya kwanza iitwayo NURU, Akiongea na Blog hii Silvanus Mumba ambaye pia ni Muubiri na Muinjilist amesema Album yake ina nyimbo 8 ambazi Mungu alimuonesa na kumtaka aimbe ili watu wapatekupokea uponyaji wa kiroho na kimwili

Mumba alisema Watu wainunue Album yake wasikie kilicopo kwani anasema Nyimbo yake ya kwanza iitwayo NITASUBIRI ilifanya vizuri sana na kumfanya ajisikie Faraja  kwa Mapokezi mazuri, ambayo Watanzania na Washabiki wa mziki wa Injili Duniani waliupokea na kuusifu kuwa ni wimbo Bora



Ziko nyimbo nyingi Kali na Nzuri sana kwa kuzisikia, kuburudika, na kujifunza, munapokea uponyaji kupitia Wimbo mmojammoja ulioimbwa katika Album yangu anasema Silvanus

Kuusikia Wimbo wa Kwanza uitwao Nitasubiri check hapa,

NITASUBIRI - SILVANUS MUMBA

Kuipata AlbumhiiMpigie moja kwa moja Mtumisi wa MunguSilvanus Mumba kupitia
Simu: 0713073280

Wasiliana naye kupitia
Facebook @revmumba
Instagram @silvanusmumba
Twitter      @silvanusmumba

Jun 27, 2017

TAMASHA LA DADA JACKLINE SKAMWA, KUFANYIKA JUMAPILI HII 2/07/2017

Akiongea na Mwandishi wetu, Jackline Skamwa anasena, anawashukuru sana Ndugu Silvanus Mumba (Muinjilist na Muimbaji wa Kimataifa) pia John Mgina (Kichaa wa Yesu) na Merciana Mwakapasa, Kwa kuwa naye Bega kwa bega katika maandalizi ya Uzinduzi wa Imefunguka (Mchum Yesu)

Waimbaji watakao hudumu ni wengi mno na Tamasha hilo, litakuwa la Kipekee sana, Anasema hategemei kuchangisha kitu chochote, isipokuwa atakaye Guswa na Albam yake au kupenda kuendeleza huduma hiyo, basi atamsupport kwa kununua Albam yake, ili aweze kufanya tamasha kubwa zaidi la kumtukuza Mungu.

Muimbaji Silvanus Mumba pia atakuwepo na waimbaji wa kwenye picha ifuatayo hapa chini, wote watahudumu









HAKUNA KIINGILIO, NI BUREEEEEE, NJOONI TUMSIFU MUNGU






Tamasha hili litafanyikia katika kanisa la OASIS HEALING MINISTRY (OHM) Ka Mchungaji NTEPA. KANISA  hili lipo nyuma ya Ubungo Plaza, ukifika hapo ulizia Kwa mchungaji ntepa utakuwa umefika. 
au Piga simu number 0713073280

Jun 14, 2017

BAADHI YA WAIMBAJI KWENYE TAMASHA LA BIG PRAISE CONCERT, SILVANUS MUMBA YUMO

Gazet lako la mtandaoni la Peruzi Gospel limekutana na Waandaaji wa BIG PRAISE Concert ambalo litafanyika Jumapili hii tarehe 18June 2017 Pale FPCT kurasini. Tamasha hili limekuwa Gumzo kubwa Nje na Ndani ya Nchi kwa jinsi maandalizi yake yalivyo pamba moto na kuchukua hisia za watu mbali mbali wa kubwa kiasi kwamba hata viongozi wa kisiasa kuliongelea kuwa ni Tamasha litakalo tikisa jiji na Tanzania kwa ujumla.

Wametaja list kubwa sana ya waimbaji lakini Muimbaji wa kimataifa SILVANUS MUMBA, EMMANUEL MBASHA, BISHOP ABRAH, BEATRICE KITAULI, BAHATI SIMWICHE NI BAADHI YAO, KUPATA LIST MAMILI ANGALIA PICHA HAPA CHINI WOTE WATAKUWEPO KATIKA KUFANYA KAZI INAKAMILIKA













HAKIKA TUTAUONA UWEPO WA BWANA TAMASHA HILI SIO LAKUKOSA KABISA, MAANA MAPRODUCER, MADIRECTOR NA WADAU WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA WATAKUTANA NA WAIMBAJI NA WAHUBIRI INJILI KATIKA STAGE MOJA. KIINGILIO NI BURE KABISA

MUMBAJI WA INJILI TANZANIA SILVANUS MUMBA AGEUKA KUWA DILI

Muimbaji wa Nyimbo za Injli Tanzania ajulikanaye kwa jina la Silvanus Mumba, aka Reverent Silvanus Mumba, amekuwa Deal au Talk of the Town nchini Zambia, Congo, Malawi na South Africa, Baada ya Tamasha lake alilo lifanya Hivi Karibuni Ndola nchini Zambia.

Akiongea na Muandishi wetu hapa Zambia, alisema anapendwa kwa nyimbo zake ambazo zimewekwa vionjo vya kizazi kipya na yeye anabarikiwa sana na uimbaji wake binafsi, lakini pia kupitia huduma yake ya uimbaji wengi wamepata kuokolewa na wengine kupata uponyaji. 

Silanus amsema Albam yake ipo tayari na soon itakuwa released, anacho subiri ni Uongozi wake umruhusu tu aanze mchakato ili watu wapate kuburudishwa na vibao vilivyopo katika Albam hiyo. 

Mimbaji huyo ambaye anamuonekano mzuri (HB) amesema anapata usumbufu mkubwa sana especial kwa wasichana wanaojigonga kwakwe ili wamteke kimapenzi, lakini yeye anamsimamo mmoja tu, anafanya sanaa ya uimbaji kwaajiri ya Kumtukuza Mungu hivyo mambo mengine hawezi kuyachanganya katika kazi yake.  

Aidha Silvanus amesema kwa sasa yuko chimbo kuandaa Albam yake ya pili yenye vibao vikali hatari, ambavyo ataanza kuviachia mwezi December mwaka huu, huku akiwaomba washabiki wake wa nchi za jirani wakae mkao wa kula. alipo ulizwa kwanini Tanzania hakubaliki sana alijibu kuwa Nabii awiki nyumbani ingawa na nchini Tanzania anamatamasha makubwa mawili ambayo amesema lazima atafanya mabalaa makubwa sana ili watu wajifunze kupitia yeye. 

Matamasha hayo ni BIG PRAISE CONCERT  na TAMASHA LA SIFA AMBAYO imembidi asimamishe shughuli zake zote kwaajiri ya kujiandaa na Matamasha hayo, Muimbaji huyo amesema waandaaji wengi wa Matamasha wanamuogopa kutokana na status yake na Elimu yake, lakini amewatoa hofu kuwa Kwenye uimbaji status ya maisha inakaa pembeni na Gharama za kumchukua si kubwa kama wanavyo fikiria,

Silvanus Mumba anapatikama kwa Contacts:  
WHATSAPP:   0713073280
FACEBOOK:     Silvanus C. Mumba 
INSTAGRAM: silvanusmumba


Peruzzi na Mimi.

Oct 1, 2016

THE SONG IS NITASUBIRI


THE MAN OF GOD, REV SILVANUS MUMBA
RELEASED HIS NEW VIDEO NAMELY "NITASUBIRI" The song is full of blessings, and allot of inspirations, it is insisting about to wait for the Gods blessings since are there for us.